ARUSHA JOURNALISM TRAINING COLLEGE

ARUSHA JOURNALISM TRAINING COLLEGE
CHUO BORA CHA UANDISHI WA HABARI TANZANIA

Saturday, January 30, 2016

WAZIRI MKUU MAJALIWA AONGOZA MBIO ZA HAPA KAZI TU DODOMA HALF MARATHON

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiongoza mbio za Wabunge za Hapa Kazi Tu Dodoma Half Marathon zilizoanzia Bungeni hadi uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma Januari 30, 2016. Kushoyo kwake ni Waziri wa Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye na kushoto ni Naibu Spika wa Bunge, Dkt Tulia Ackson. Mwansasu (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
Baadhi ya Washiriki wa mbio za Hapa Kazi Tu Dodoma Half Marathon wakishiriki mbio hizo mjini Dodoma Januari 30, 2016.
Mmoja wa wapigapicha walioshiriki mbio za Hapa Kazi Tu Dodoma Half Marathon alilazimika kuomba msaada kwa askari wa usalama barabarani Mjini Dodoma Januari 30, 2016. 
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi ufunguo wa pikipiki mshindi wa kwanza wa mbio za Hapa Kazi Tu Dodoma Half Marathon upande wa wanaume, Emmanuel Giriki kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma Januari 30, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi zawadi ya Pikipiki mshindi wa kwanza upande wa wanawake wa Mbio za Hapa Kazi Tu Dodoma Half Marathon, Angela Davile (kulia) kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma Januari 30, 2016.
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Benki ya CRDB tawi la Dodoma ambao wamedhamini pambano la mpira wa miguu kati ya wabunge na benki hiyo kwenye uwanja wa Jamhuri Januari 30,2016. Benki hiyo pia ilitoa vifaa vya michezo kwa timu ya Bunge. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu) 

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemtaka Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kuandaa kikao cha haraka na viongozi wa vyama vya michezo nchini ili wamueleze kila mmoja amejipanga vipi kuinua viwango vya michezo katika chama chake.

Ametoa agizo hilo leo mchana (Jumamosi, Januari 30, 2016) wakati akizungumza na mamia ya viongozi na wakazi mbalimbali wa mkoa wa Dodoma ambao walishiriki mashindano ya mbio za nusu marathon (km. 21 na km. 5) zilizofanyika leo mjini Dodoma.

Mashindano hayo yalijulikana kama “HAPA KAZI TU HALF MARATHON” yamefanyika ikiwa ni sehemu ya kuhimiza uchapakazi miongoni mwa Watanzania lakini pia ni sehemu ya maandalizi ya kuelekea kuadhimisha siku 100 za utendaji kazi tangu Rais John Pombe Magufuli alipoapishwa na kuanza kazi.

“Kuna maboresho yanaendelea ndani ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo lakini haya yote hayawezi kufanikiwa kama viongozi wa michezo hawajajipanga vizuri. Ninatakata niandaliwe kikao cha siku moja na viongozi wa vyama vya michezo nchini ili waje wanieleze kila mmoja amejipanga vipi kuinua hali ya mchezo wake,” alisema huku akishangiliwa.

Alitumia fursa hiyo kuupongeza uongozi wa Shirikisho la Riadha Tanzania kwa kuandaa mbio hizo muhimu za kuhimiza Watanzania kuchapa kazi, lakini pia ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya kushiriki katika mashindano ya Olimpiki yatakayofanyika baadaye mwaka huu huko Rio de Janeiro, Brazil.

“Tunataka tuondokane na kauli ya Tanzania kuwa ni kichwa cha mwendawazimu na nipende kusisitiza kuwa maandalizi haya yasiwe ya mwisho bali yawe ya muda mrefu kwa sababu tunaenda kushiriki mashindano ya dunia. Nasema tena, tuache utamaduni wa maandalizi ya kukurupuka,” alisisitiza.

Aliwataka wadau mbalimbali wajitokeze kusaidia taasisi za michezo.

Waziri Mkuu Majaliwa ambaye alishiriki mbio za km. 2.5 kuanzia saa 1 asubuhi, alikimbia kutoka eneo la Bunge hadi uwanja wa Jamhuri na kuzindua mashindano ya km. 21 saa 1:47 asubuhi na yale ya km. tano aliyazindua saa 1:51 asubuhi.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu alikabidhi pikipiki aina ya GSM kwa washindi wa kwanza wa nusu marathon, mabati 100 kwa washindi wa pili na mabati 40 kwa washindi wa tatu. Mshindi wa tatu hadi wa 10 kwa wanawake na wanaume walikabidhiwa fedha taslimu.

Washindi wa kwanza hadi wa tatu waliokabidhiwa zawadi na Waziri Mkuu upande wa wanawake ni  Anjelina Daniel (Pikipiki); Fadhila Salum (mabati 100) na Catherine Lange (mabati 40). Wote wanatoka mkoa wa Arusha.

Kwa wanaume walioshinda nafasi kama hizo ni Emmanuel Giniki (Katesh, Babati) aliyeshinda pikipiki; Gabriel Gerald wa Arusha (mabati 100) na Fabian Joseph wa Arusha (mabati 40).

Wakati huo huo, Benki ya CRDB Dodoma ilitoa zawadi za sh. 250,000/- kila mmoja kwa washiriki watatu ambao ni walemavu walioamua kushiriki mbio hizo mwanzo hadi mwisho. Waliokabidhiwa zawadi hizo na Waziri Mkuu ni Bw. Hassan Hussein Sharif, Bw, Christian Ally Amour na Bw. Shukuru Khalfani.

Benki hiyo ilikabidhi pia vifaa vya michezo kwa ajili ya timu ya wabunge kwa ajili ya pambano la soka linalotarajiwa kufanyika leo saa 10 jioni kwenye uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma baina ya timu ya Bunge na timu ya CRDB. 

Dkt. Kigwangalla awapa funzo watumishi wa sekta ya afya, awataka kuwa wabunifu


Licha ya juhudi zinazofanywa na serikali kuboresha sekta ya afya nchini, watumishi wa sekta ya afya wametakiwa kuwa wabunifu ili kuweza kutoa huduma kwa watu wote hususani wenye kipato cha juu.
IMG-20160130-WA0029
Licha ya kutembelea wodi mbalimbali za wagonjwa, Dkt. Kigwangwala alitembelea maabara ya hospitali hiyo na kuridhika na vifaa vilivyopo kwenye hospitali, kushoto ni mtaalamu wa viwango vya maabara, Felix Zelote akimpatia maelezo waziri huyo
IMG-20160130-WA0030
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla akibadilishana mawazo na wataalamu wa hospitali hiyo kwenye chumba cha upasuaji
Hayo yamesemwa leo na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla wakati akitembelea Hospitali ya Mount Meru iliyopo mkoani Arusha.
Amesema hospitali zinatakiwa kusimama zenyewe kwa ukusanyaji wa mapato,hivyo upo ulazima wa kujenga au kukarabati majengo ambayo wanaweza kufanya wodi za kulipia ambazo zitakua zenye ubora ambao unaweza kuwashawishi watu wenye pesa kuja kupata huduma kwenye hospitali za umma kuliko hivi sasa wanakimbilia hospitali binafsi.
"Hii itaifanya serikali kupata pesa ambazo sehemu kubwa zitatumika kuwahudumia watu wenye kipato cha chini hospitalini hapa,” alisema Dkt. Kigwangalla.
Hata hivyo Naibu Waziri huyo alisema wateja wengi wanapokuja kupata huduma kwenye vituo vya huduma ya serikali,wanakata tamaa kwakuwa wanakuta hakuna watoa huduma, dawa wala vifaa tiba hivyo wanakimbilia huko kwenye hospitali binafsi.
"Lengo letu sio kuua hospitali binafsi bali tunataka muimarishe huduma za kulipia ili tupate pesa za kuwahudumia wasio na uwezo na ninyi watoa huduma wa serikali mpate sehemu yenu ili muweze kufanya kazi kwa ufanisi,” alisema Dkt. Kingwangalla.
IMG-20160130-WA0032
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla akibadilishana mawazo na wataalamu wa hospitali hiyo kwenye chumba cha upasuaji
IMG-20160130-WA0027
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangwala akiwa amembeba mtoto mchanga (bado hajapatiwa huduma) na mama wa mtoto huyo Bi. Jamila Petro alipotembelea wodi ya wazazi hospitalini hapo
IMG-20160130-WA0028
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla akimuangalia mtoto huyo

RAIS MAGUFULI AWAAPISHA MNADHIMU MKUU WA JWTZ, BALOZI WA TANZANIA KUWAIT NA KATIBU TAWALA WA KATAVI NA MWANZA LEO IKULU DAR ES SALAAM


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimuapisha Dkt. Mahadhi Juma Maalim kuwa Balozi wa Tanzania  Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimkabidhi nyezo za kazi Dkt. 
Mahadhi Juma Maalim baada ya kumuapisha kuwa Balozi wa Tanzania  Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimuapisha  Luteni Jenerali Venance Salvatory  Mabeyo  kuwa Mnadhimu Mkuu wa JWTZ  Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimkabidhi nyezo za kazi Luteni Jenerali Venance Salvatory Mabeyo baada ya kumuapisha  kuwa Mnadhimu Mkuu wa JWTZ baada ya kumuapisha kuwa Balozi wa Tanzania  Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimuapisha Kamishna wa Polisi Clodwig Mathew Mtweve  kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza  Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimkabidhi nyezo za kazi Kamishna wa Polisi Clodwig Mathew Mtweve bvaada ya kumuapisha  kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza  Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akipokea saluti toka kwa Kamishna wa Polisi Paul Amani Moses Chagonja kabla ya  kumuapisha kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimuapisha Kamishna wa Polisi Paul Amani Moses Chagonja kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimkabidhi nyezo za kazi Kamishna wa Polisi  Paul Amani Moses Chagonja baada ya kumuapisha kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiongea na Mnadhimu Mkuu wa JWTZ MStaafu Luteni Jenerali (Rtd) Samuel Albert Ndomba baada ya shughuli ya kiapo Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akifurhia jambo  na Mnadhimu Mkuu wa JWTZ MStaafu Luteni Jenerali (Rtd) Samuel Albert Ndomba baada ya shughuli ya kiapo Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue na viongozi wa Jeshi la Wananchi na Jeshi la Polisi  katika picha ya pamoja baada ya kuapishwa Mnadimu Mkuu wa JWTZ, Balozi wa Tanzania Kuwait na  Katibu Tawala wa Mikoa ya Katavi na Mwanza Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimpongeza  Kamishna wa Polisi Paul Amani Moses Chagonja baada ya  kumuapisha kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimpongeza Luteni Jenerali Venance Salvatory Mabeyo baada ya kumuapisha  kuwa Mnadhimu Mkuu wa JWTZ baada ya kumuapisha kuwa Balozi wa Tanzania  Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimpongeza  Kamishna wa Polisi Clodwig Mathew Mtweve baada ya kumuapisha  kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza  Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akimpongeza  Dkt. Mahadhi Juma Maalim baada ya kumuapisha kuwa Balozi wa Tanzania  Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  na viongozi wa Jeshi la Wananchi na Jeshi la Polisi  katika picha ya pamoja baada ya kuapishwa Mnadimu Mkuu wa TPDF, Balozi wa Tanzania Kuwait na  Katibu Tawala wa Mikoa ya
 Katavi na Mwanza Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akipena mikono na Mkuu wa Majeshi Jenerali Davis Mwamunyange  baada ya kuwaapisha Mnadimu Mkuu wa TPDF, Balozi wa Tanzania Kuwait na  Katibu Tawala wa Mikoa ya Katavi na Mwanza Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akipena mikono na Inspekta Jenerali wa Polisi Afande Ernest Mangu baada ya kuwaapisha Mnadimu Mkuu wa TPDF, Balozi wa Tanzania Kuwait na  Katibu Tawala wa Mikoa ya Katavi na Mwanza Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiwa na Mnadhimu Mkuu wa JWTZ mpya  Luteni Jenerali Venance Salvatory  Mabeyo  na  Mnadhimu Mkuu wa JWTZ  Mstaafu Luteni Jenerai (rtd) Samwel Ndomba Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016
 Mnadhimu Mkuu wa JWTZ mpya  Luteni Jenerali Venance Salvatory  Mabeyo  na  Mnadhimu Mkuu wa JWTZ  Mstaafu Luteni Jenerai (rtd) Samwel Ndomba Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli  akifurahia jambo na viongozi wa Jeshi la Wananchi na Jeshi la Polisi  baada ya kuwaapisha  Mnadhimu Mkuu wa JWTZ, Balozi wa Tanzania Kuwait na  Katibu Tawala wa Mikoa ya Katavi na Mwanza Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufulia akiongea na viongozi  baada ya kuwaapisha Mnadimu Mkuu wa TPDF, Balozi wa Tanzania Kuwait na  Katibu Tawala wa Mikoa ya Katavi na Mwanza Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akiongea na   Kamishna wa Polisi Paul Amani Moses Chagonja baada ya  kumuapisha kuwa Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016
  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na msemaji wa JWTZ Luteni Kanali Ngeleba  Lubinga baada ya kuwaapisha Mnadimu Mkuu wa TPDF, Balozi wa Tanzania Kuwait na  Katibu Tawala wa Mikoa ya Katavi na Mwanza Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Joseph Magufuli akisalimiana na Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi Abdulrahman Kaniki baada ya kuapishwa Mnadimu Mkuu wa TPDF, Balozi wa Tanzania Kuwait na  Katibu Tawala wa Mikoa ya Katavi na Mwanza Ikulu jijini Dar es salaam leo January 30, 2016

Thursday, January 28, 2016

HOTUBA YA NYERERE DHIDI YA VIONGOZI WAADILIFU.

Andrew Chenge Asema Haya Kuhusu Sakata la Tegeta Escrow Baada ya Kuchaguliwa Kuwa Mwenyekiti wa Bunge



ANDREA NGOBOLE


MBUNGE wa Bariadi, Andrew Chenge na wabunge wawili wa Viti Maalumu, Dk Mary Mwanjelwa na Najma Giga, wamechaguliwa kuwa Wenyeviti wa Bunge kwa kipindi cha miaka miwili na nusu.

Uchaguzi huo ulifanyika jana baada ya majina yao kupendekezwa na Kamati ya Uongozi na kuyawasilisha bungeni kwa ajili ya uchaguzi.

 Katika uchaguzi huo, uliotanguliwa na wabunge hao kujieleza mbele ya wenzao na kuulizwa maswali, sakata la Tegeta Escrow liliibuka baada ya Chenge kujieleza.
“Katika Bunge lililopita, chama chako na wabunge walikuwajibisha kwa kashfa ya Escrow, je, siku ukiliongoza Bunge na hoja ikarudi ndani uko tayari kuisimamia,” Mbunge wa Ndanda, Cecil Mwambe (Chadema) alimuuliza Chenge.

Akijibu swali hilo, Chenge alisema Bunge linaongozwa na Kanuni na itakapokuja mbele ya Bunge au kwenye Kamati, ikaonekana kuna maslahi ama inamhusu mbunge, ni busara kuzingatia kanuni nafasi hiyo ikaachwa mwingine aifanye shughuli za Bunge zisiwe na makandokando ya aina yoyote.
“Naona niishie hapo, ningeweza kusema zaidi ya hapo,” alisema Chenge ambaye alikuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa zaidi ya miaka 10 na pia Mwenyekiti wa Kamati ya Bajeti ya Bunge la 10 kabla ya kujiuzulu kutokana na sakata la Tegeta Escrow.

Awali akijieleza Chenge ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo, alisema “napenda niliahidi Bunge na Watanzania kwa ujumla, kwamba hii ni dhamana nzito ya kumsaidia Spika na Naibu.
“Lakini niwahakikishie nitatekeleza jukumu hilo kwa uadilifu, na kwa uaminifu ili nitende haki inayoonekana na bila chuki, wala upendeleo wowote kwa faida ya kujenga misingi bora ya Bunge hili lakini pia kwa kuwatumikia Watanzania wote,” alisema.

Kuhusu swali la Mbunge wa Nsimbo, Richard Mbogo (CCM) aliyetaka kufahamu ni namna gani Chenge atadhibiti matumizi ya lugha ya kuudhi au kudhalilisha wengine, Chenge alisema Kanuni za Bunge kama zilivyo sheria za nchi, zinakata pande zote kama ilivyo msumeno.

Alisema ikithibitika kwamba mbunge amekiuka kanuni, kiti kitazingatia baada ya kupima kauli na maelezo aliyotoa bungeni.

“Baada ya kupima, tuhakikishe kwamba tunayosema humu bungeni yawe ya kweli, kweli tupu yasiwe ya uongo,” alisisitiza.

Mwanjelwa ambaye ni Mbunge wa Viti Maalumu mkoani Mbeya, katika kujieleza mbele ya wabunge, aliomba wamwamini na kuahidi kuwatumikia bila kujali itikadi kwa faida ya wananchi wote.

Mwanjelwa alikiri kwamba Bunge hili lina changamoto nyingi, lakini atakachozingatia ni utaifa kwanza.


Najma, ambaye kitaaluma ni Mwanasheria, aliahidi kuwa msaada mkubwa kwa Spika. Aliahidi kuwa atahakikisha anaweka maslahi ya taifa mbele kwa kutoa haki sawa kwa wabunge wote bila kujali vyama vyao.


Spika wa Bunge, Job Ndugai alihoji kwa pamoja wanaoafiki mapendekezo ya Kamati ya Uongozi, ndipo wabunge walio wengi wakaridhia Chenge, Mwanjelwa na Najma wawe wenyeviti. Wenyeviti wa Bunge hufanya kazi wakati ambao Spika au Naibu Spika wakiwa hawapo bungeni.


Katika Bunge la 10, wenyeviti walikuwa Mussa Azzan Zungu, Kidawa Himid Saleh, Lediana Mng’ong’o, Muhammed Seif Khatib, Sylvester Masele na Jenista Mhagama.


Kwa mujibu wa Ndugai, Kamati yau Uongozi imejiwekea utaratibu wa kupendekeza majina na ilipokutana chini ya uenyekiti wa spika, iliamua kuwapendekeza wabunge hao watatu ambao wote ni kutoka CCM

Thursday, January 21, 2016

ANGALIA HISTORIA NZIMA YA RAISI WA AWAMU YA TANO WA TANZANIA MHESHIMIWA MAGUFULI

        

Hii ni moja ya historia ya Raisi aliyeingia madarakani hivi karibuni na kutumbua majipu ya watendaji wasio waaminifu

TIZAMA HOTUBA NZIMA YA UFUNGUZI WA BUNGE LA JMT YA MHESHIMWA RAISI MAGUFULI HAPA

HABARI PICHA MBUNGE WA MONDULI MHESHIMIWA KALLANGA ALIPOZURU MTO WA MBU KUSHUHUDIA UHARIBIFU MKUBWA WA MAZAO

mbunge wa monduli bwana Julias Kallanga akiangalia mashamba yaliyoharibiwa na upepo mkali ulioharibu mashamaba haoy eneo la mto wa mbu mkoani Arusha. ameiomba serikali kutoa msaada wa chakula kwa kaya zaidi ya mia mbili ambazo zipo hatarini kukosa chakula kutokana na uharibifu huo

hapa akiwapa moyo wamoliki wa mashamba hayo na jinsi ya kuweza kujikwamua na tatizo hilo linaloikabili jamii hiyo ya watu wa mto wa mbu

SERIKALI YAOMBWA KUCHANGIA CHAKULA CHA WATOTO WAKIWA SHULENI.



SERIKALI yaombwa kuchangia chakula cha watoto wakiwa shule ili kuwasaidia kusoma wakiwa wameshiba kwani watoto hawawezi kusoma wakiwa na matumbo hayana chakula.

Hayo yamesemwa na Shule kuu ya Elimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Joviter Katabaro wakati akichangia maada katika mkutano wa kujadili masuala ya elimu katika mkutano uliofanyika katika ukumbi wa Mwalimu Nyrere jijini Dar es Salaam leo.

Nae Mkurugenzi mtendaji wa shirika la Haki Elimu, John Kalage kuwa wamependekeza Lugha ya Kiswahili na Kiingereza iwe lugha ya kufundishia na kujifunzia kwa ngazi zote ili kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia.

Pia ametoa wito kwa serikali kuwa kutoa elimumsingi bure sabamba na kupunguza michango ya wazazi mashuleni.

Aidha Karage  amesema kuwa ili kuhakikisha ubora mashuleni, shule, taasisi na vyuo vinapaswa kufanyiwa ukaguzi kuhusu ufundishaji na ujifunzania pamoja na mazingira kuwa mazuri.
Mhadhiri wa chuo kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Bashiru Ally akizungumza na wadau wa elimu leo jijini Dar es Salaam wakati wakijadiliana kuhusiana na masuala mbalimbali ya elimu kwa watoto waliotolewa fedha na Serikali kwaajili ya kutolewa elimu bure kwa elimu ya Sekondari na Shule za msingi. Kulia ni Profesa Mshiriki wa chuo kikuu cha Dodoma, Profesa Willy Komba.
Profesa Mshiriki wa chuo kikuu cha Dodoma, Profesa Willy Komba akizungumza na wadau wa Haki elimu leo wakati wa kijadili Lugha gani itumike katika kufundishia kwa wanafunzi wa shule za hapa nchini.ilikwa alisema sema kuwa wanafunzi wasichanganyikiwe kuhusiana na lugha ambayo itatumika kufundishia kwa masomo yao.
Meneja wa Idara ya Utafiti na uchambuzi wa Haki Elimu akizungumza na wadau wa elimu leo katika ukumbi wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam leo. Kulia ni Shule kuu ya Elimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Joviter Katabaro akiwa katika mkutano huo wa wadau wa elimu.
Profesa Mshiriki Chuo kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Martha Qorro akizungumza katika uzinduzi wa ripoti ya haki elimu iliyozinduliwa leo katika ukumi wa mwalimu nyerere jijini Dar es Salaam kuhusiana na namna gani serikali itoe uchangauzi wa pesa zilizotolewa kwa shule za msingi na sekondari zitumikwa kwa namna ani na mawanyo wake upoje ili kila mwananchi ajue hizo pesa zimetolewa kwa matumizi gani.
Baadhi ya wadau wa elimu wakiwa katika mkutano huo wa kujadili masuala ya elimu uliofanyika jijini Dar es Salaam leo

Picha na Avila Kakingo wa Globu ya Jamii